Wakati sio sumu |

Wakati sio sumu

iliyoandikwa na Erich Brandeis


Hapa kuna kitu cha kuongezwa kwa hazina yetu – nyumba ya umaksi na kuandaliwa na kuwekwa kwenye ukuta wa kila nyumba. Kama wamaksi wengi na methali sio sahihi kwa kikamilifu. Lakini ni sawa tu kwangu kwa sababu nimeijaribu na nikaona ni kweli.

Ijaribu mwenyewe na inaweza kufaidi. Wacha bibi yako ajaribu – unajua wakati upi. Usijali Watoto, hawahitaji, sio kwa sasa. Ndio hii: “WAKATI SIO SUMU.”

Si kuibuka nayo. Sijui nani alifanya. Lakini ilikuwa maada kuu katika koongamano la madaktari na wapasuaji Cincinnati.

Kulingana na wale madaktari, malalamishi makuu kutoka kwa wagonjwa wao ni: “Daktari, ninazeeka.” Halafu wanalaumu karibu kila kitu kinachowatendekea kwa uzee. Wanafikiria hakuna kitu ambacho wanaweza Fanya juu yake. Wanafikiria ugonjwa wa yabisi, shida za moyo, saratani, kwa kweli kila kitu ni kwa sababu ya mda. Upuuzi, wanasema madaktari. Wakati hauna uhusiano wowote na haya. Acha ninukuu kutoka kwa hotuba iliyofanywa katika koongamano na mtaalamu maarufu:

Kila kiungo cha mwili kimepewa uwezowa maisha ya milele wakati kwa kutosha kimepewa chakula, hewa na joto inayofaa na wakati kuondolewa kwa taka inafanywa kwa maakini. Wakati hauna athari kwa viungo vya mwili vilivyohifadhiwa kwa hali kama zile au kwa kweli kwa viungo vya mwanadamu katika hali yoyote.

“ Nguvu sio kwa lazima haitofautiki kulingana na umri wa mtu mzima. Inatofautiana moja kwa moja na sababu za urithi, maisha yenye afya, hali ya akili, na matibabu na upasuaji.”

Madaktari walikubaliana ya kwamba Imani katika athari za wakati huenda zikapunguza hima; kwa hivyo matarajio na juhudi zinakatizwa. “ Wale wote wanaendeleza neurosis wamesajiliwa kwa ushirikina mkali ya kwamba wakati kwa njia Fulani ni sumu inayoshinikiza kitendo cha siri kinachojumlisha.”

Ripoti inaendelea kusema ya kwamba wakati kuna neurosis ya wakati, ujasiri na matumaini zinapungua, kuendelea kwa wasiwasi kunapunguza ufanisi, na kuongeza wasiwasi na kukasirika.”

Dalili za kufikiriwa zinatambuliwa kwa kuongezeka kwa ukali. Akili au moyo inaonekana kudidimia. Umaakini wa ajabu unapatiwa kila dalili ndogo.

Na kwa hakika, wale madaktari wako sawa. Nimekuwa na uchungu mbaya kwa shingo. Uchungu mkali. Gouti? Neuritis? Uzee? Nikachunguza. Unajua ilikuwa nini? Kipini ambacho dhobi aliweka.

Natumai utafaidika na makala hii. Lakini kipande kidogo cha ushauri wa kuondoka. Usiende ukisherehekea hapa na pale ya kwamba madaktari wamesema uzee ni wa kufikiria. Na usijifanye nguruwe. Nguruwe hawaishi sana.