Tengeneza nafasi kwa Mungu ndani ya moyo wako
Iliyoandikwa na MARY BETH SINGLETERRY
Niliguswa sana na wimbo ambao sikuufahamu unaoitwa, “ Tengeneza nafasi kwa Mungu ndani ya moyo wako.” Moja ya mistari ilikuwa, “kuna nafasi katika moyo wako kwa Mungu kuandika hadithi yake, na kubadilisha ndoto zako kwa utukufu wake?” Wimbo ule uliendelea kuuliza lile swali, kuna nafasi katika moyo wako?
Nilifikiria ya kwamba ukuaji wowote nimepata katika Sayansi imekuwa kwa sababu nilihitaji kufanya nafasi katika moyo wangu ndio Kristo aje. Sisi wote tunahitaji kubadilisha ndoto zetu, mipango yetu ya kimakusudi, au hisia zetu za maisha ni nini, kwa mapenzi ya Mungu katika maisha yetu, na hisia ya kweli ya kiroho ya kile maisha ni.
Hata katika mwanzo, ukifikiria uko na nafasi tu kidogo katika moyo wako, unavyokua na kuchukua huo ukweli, unapata moyo wako unapanuka zaidi na zaidi, na hivi karibuni huo upendo wa Mungu unafurika kupitia kwako, na umefanya nafasi ndani ya moyo wako kwake. Ndoto hizo zote za kimwili za zamani zote ni za utukufu wake.
Nilisoma kitu cha kupendeza sana hivi karibuni kuhusu Handel, aliyeandika Masihi mzuri, ambayo wengi wetu waliisikiliza wakati huu wa mwaka. Aliandika kwa muda mfupi sana, na kabisa ilikuwa ni msukumo wa kimungu. Alisema ilikuja kupitia yeye. Alipatiwa aya hizi nzuri za kuandikia mziki. Alisema alitokwa na machozi alipoandika kipande cha wimbo “ Haleluya” kwa sababu alihisi ni kama ameiona sura ya Mungu, alafu alipata tajiriba ya mguso wa mbinguni kupitia mziki ule mzuri. Masihi wa Handel amefikia watu wengi. Hata watu ambao kamwe hawajawai kuamini Mungu na wakati wanasikia muziki ule mtakatifu, na maneno yale matakatifu, wanazipata zikiwa za kuinua na zenye nguvu. Wakati Handel alisifiwa kwa yale aliyoyafanya, alisema, “ Nampatia Mungu utukufu wote.” Ni hadithi nzuri sana.
Zote tuko hapa kumpatia Mungu nafasi katika mioyo yetu. Hakuwezi kuwa na kusudi lililo na utukufu kushinda hii.