Kusudi letu la maisha
Ambayo Imeandikwa Na Martha Wilcox
Mama Eddy anarekodi kusudi la maisha yake anaposema, ” Kusudi la maisha yangu ni kuvutia wanadamu na utambuzi wa kweli wa kazi kwa vitendo ya Sayansi ya Kikristo.”
Hakukuwa na shauku katika akili ya Bi Eddy ya kwamba alikuwa na kusudi kamilifu katika maisha yake kutimiza, na kusudi ilikuwa nini. Haijalishi ni nini wengine wangefanya, ilikuwa dhahiri imeimarika na imefanikiwa katika mawazo yake, na alijua lazima afuate mwelekeo huu dhabiti maishani ndio aweze kutimiza kusudi lake la Kimungu.
Tunapotambua ukuu wa kusudi lake, imemaanisha nini katika maisha yetu kuwa na Sayansi isiyoshindwa na inayofanya kazi kila wakati kuitumia katika shughuli zetu za ubinadamu, tunaweza shangaa na kudhihirisha shukrani zetu kwa baraka hii ambayo imetokea kwetu katika ulimwengu wetu.
Mama Eddy alikuwa na hisia safi ya maana ya ijulikanayo kama tajiriba ya mwanadamu. Alitambua ya kwamba hakuna aliyezaliwa nje ya wakati unaofaa. Alijua ya kwamba alikuwa na kusudi kamilifu la kutimiza na alijua alikuwa na nguvu na hekima kutoka kwa Mungu ambayo angeitumia kutimiza kusudi ile.
Je tuko macho kama wanasayansi wa Kikristo kwa ukweli ya kwamba pia sisi tuko na kusudi kamilifu la maisha? Je tunafuata mwelekeo maalum katika maisha ili kutimiza huu uwepo wa Kimungu?
Tunatakiwa tuwe wafikiri wa kina, na tuwe na maono ya siku za furaha zaidi kwa familia ya kibinadamu. Kama wanasayansi wa Kikristo binafsi, tunahitaji upendo mkubwa wa Mungu na upendo mkubwa kwa binadamu katika roho zetu, ndio maisha bora na kusudi ifanyike . Kila mmoja wetu ako na kusudi kuu kutekeleza. Tunapaswa kuishi hivyo, na hivyo kependa, ya kwamba Mungu au ukweli ipate kueleweka kwetu na ndio tuweze kusikia sauti yake ikisema , “Hii ndio njia, tembeeni ndani yake.” { Isaya 30:21 }