Maazimio ya siku
Kutoka kwa Mashairi iliyoandikwa na Mary Baker Eddy – Ukurasa 32 Iliandikwa katika Usichana
Kuamka asubuhi na kupiga picha ya mandhari –
Nyumbani ninako ishi katika bonde, Michikichi ambao harufu yake na mvuto,
Ni mpya kila wakati
Zimetapakaa kando ya mlima;
kutazama mionzi ya jua ikiwasha anga- Maisha ya juu kuikaribisha –
Mwangaza unaoangazia jicho langu la kiroho
Na inahamasisha kalamu yangu ninapoandika;
Kufanya maazimio kwa nguvu kutoka juu, Sheria za kimwili kutii,
Kama sababu na hamu, radhi kukataa Kwamba afya naomba juhudi zangu zilipwe;
Kupiga magoti kwenye madhabahu ya rehema, Kwamba msamaha na neema kupitia mwanaye, Na zifariji roho yangu siku zote za uchovu, Zinifurahishe na matumaini kama imefanyika;
Kukumbuka baraka zangu kila siku na malipo, Na kuifanya hii ombi langu la unyenyekevu; Ongeza imani yangu na maono yangu ongeza,
Na unibariki na ahadi ya Kristo ya pumziko;
Kila saa kutafuta ukombozi wenye nguvu Kutoka kwa ubinafsi, utenda dhambi, ukosefu,
Kutokana na ubatili, upumbavu, na yote ambayo ina makosa – Kwa malengo yanayotufunga kwa dunia;
Kwa hisani kuputia juu ya kidonda, au adui
{ Na kumbukumbu kuachana kwa mda}, Kupumua ombi kwamba upendo niujue, Huruma zake huzuni yangu hudanganya, –
Kama maazimio haya yanatendwa,
Na imani inasambaza maoni yake ng’ambo,
Pambo tamu nikifikiria siku vile ni chache,
Zinazonielekeza kwa Mungu wangu.