Ajira |

Ajira


Mojawapo ya shida za kibinadamu ambayo imedhamiri ni ajira. Hata wale ambao hawategemei kazi yao kwa mkate wa kila siku wako na tatizo hili kulitatua.

Mwandishi alikuwa kwa hali kama hii ambapo ajira ilikuwa ni hitaji la lazima. Alijaribu njia zote za kawaida za kupata ajira bila ufanisi. Kulionekana kuwa na uhaba wa kazi kote nchini.

Asubuhi moja nikiomba katika masaa tulivu ya asubuhi, wazo likanijia kwa uwazi ya kwamba haikuwa lazima ” nipate kazi” ama ninyakue ya mwingine, lakini ni kwamba nilikuwa naangaza Mungu na ilikuwa tu nielewe kwamba nafsi yangu ya kweli iliumbwa na kutawaliwa na Mungu. Kazi yangu basi ilikuwa ni dhihirisho la Mungu. Hivi karibuni baada ya kupata mwangaza huu, njia ambayo haikuwa imetarajiwa ya kazi ilifunguka.

Katika kutatua tatizo hili katika Sayansi ya Kikristo, mwanafunzi anapata kuelewa kuwa kila kitu ambacho kinachohusu ajira lazima kiinuliwe kutoka kikoa cha ijulikanayo kama mwili na kuingizwa kwa ufalme wa Mungu.

Kama vile Mama Eddy anatangaza katika Sayansi na afya {ukurasa 468}, “Yote ni Mungu aishiye milele na dhihirisho za milele,” shughuli yote halisi lazima iwe katika ufalme wa kiroho. Kisha inakuwa wazi ya kwamba yale yote mwanafunzi anawezafanya ni daima kuajiliwa kwa fikira sahihi. Yoyote kazi yake, iwe kuendesha injini au kulima shamba, ni wazo linaloelekeza kitendo.

Kutokana na msimamo huu, hakuna mtu ambaye hayuko kazini. Kama mwanafunzi anafikiria kikamilifu, akileta ” mawazo yote kwa utiifu wa Kristo,” atavuna alichokipanda, na hii itaonekana kwa njia ambayo itakidhi mahitanji ya mwanadamu sasa.

Lengo halisi la ajira kimsingi sio kupata riziki ila kumtukuza Mungu. Na Mungu hafichi huduma yake na nguvu za kuhifadhi wakati wowote. Kila wazo la kiroho linatunzwa bila kusitisha milele kote.