Kazi ya Furaha
Iliyoandikwa na ROBERT MERRITT
Labda sentesi moja muhimu sana ambayo ishawai andikwa iliandikwa na Mary Baker Eddy wakati alipojibu swali : Mungu ni nini? Aliandika: “Mungu ni isiyokuwa ya mwili, ya kimungu, mkuu kuliko yote, Akili isiyekuwa na mwisho, Roho, Kanuni, Ukweli, Upendo.” {Sayansi na Afya ukurasa 465}
Kuna sentensi ingine yenye nguvu, maono, ufumbuzi, na bado yenye uzuri wa urahisi mahali popote duniani? Lazima tutii na kutakasa majina haya matakatifu. Mama Eddy anaendelea: “Mungu. Mkuu Aliye Mimi ni; anayejua yote, anyeona yote, anayetenda yote, mwenye hekima yote, mwenye upendo wote, na wa milele; Kanuni; Akili, Nafsi, Roho; Uhai; Ukweli; Upendo; dutu yote; ufahamu.”
Kwa ajili Mungu ni mwema, Mama Eddy kwa ajabu anafafanua wema kama: “Wema. Mungu; Roho; Nguvu zote; mwenye kujua yote; mwenye uwepo wote; mwenye Kutenda yote.” Ni nguvu kipimo kipi, uzuri, afya na utawala wa kimungu ziko nyuma ya maneno haya! Zinaonyesha kiini cha anayependeza. Wajibu wetu mtakatifu na wa heshima ni kwa kuendelea kuzionyesha dhana hizi za Mungu maishani mwetu, kama wahusika wa Bibilia, Yesu, na Mama Eddy walivyofanya. Lazima tushiriki katika asili ya Mungu, kama tutatambua, utambulisho wetu wa kweli wa kiroho, kama umbo na mfano wa Mungu. Kuna Mungu mmoja, Lakini Roho mtakatifu ako na rangi na ofisi mingi. Vile tunavyomfahamu Mungu zaidi, ndivyo tunavyofahamu asili yetu ya kweli na utambulisho sahihi wa Jirani yetu.
Tunaweka uovu kando, makosa, na kuponya wagonjwa kwa kuweka katika ufahamu wetu maoni sahihi ya Mungu. Na hii ni kazi ya furaha na ya milele!