Tii Daktari Mkuu |

Tii Daktari Mkuu

Imeandikwa na Florence Roberts


Nimekuwa nikisoma Makala iliyoandikwa na Rosalie Stamp, inayoitwa “Mashauriano ya Kiroho.” Inataja mashauriano na Daktari mkuu. Inasema, kwa wakati mwingine, tunaweza tamani kama Yesu angekuwa hapa kusaidia na kuponya. Lakini inasema ingefaa tuulize , Yesu alitegemea nini kwa kazi yake ya uponyaji? Kuna vitu vitatu: alitegemea Akili ile ile ya milele, Ukweli ule ule usio onekana, Upendo ule ule mkuu wa kuokoa ambao uko nasi zote sasa.

Tunaweza kumbuka kwa wakati wote ya kwamba Daktari wetu mkuu kwa wakati wote yuko na uchunguzi mwema au hitimisho kwetu. Uchunguzi wake ni ukamilifu, uzuri ambao hutia nguvu ubinafsi wa kiroho ambao tunaakisi.

Nashukuru sana kwa haya. Ni ukumbusho ya kwamba hitimisho ya Mungu ndio ukweli, na ndio lazima sisi wote tudumishe katika mioyo yetu, hata kama akili za kimwili inasisitiza uongo na udanganyifu wake. Napenda Makala ya Mama Eddy “ Matibabu ya kila siku,” ambayo inaweza patikana katika tovuti yetu kama “Makala.” Napenda mahali anasema lazima tutangaze nyakati bila nambari, “Nimekamilika katika Mungu.” na kusema mara nyingi, “Nimekamilika, na niko na furaha.” Hii ndio inafaa kuwa matokeo ya uchunguzi wetu na hitimisho kwa sababu ndio Ukweli!