Ufahamu wa Tatizo au Ufahamu wa Suluhisho |

Ufahamu wa Tatizo au Ufahamu wa Suluhisho

Iliyoandikwa na PARTHENS


Zaburi 25, kifungu cha 10, mfano mwingine wa hali ya maumbile ya ahadi za Mungu. Inasema, “Njia zote za Mungu ni rehema na ukweli kwa wale wanaoweka ahadi zake na ushuhuda wake.”

Kila changamoto inayohitaji kukesha, maombi, na vita vya kiroho kila wakati inahitaji kusonga kwa mawazo yangu kutoka kwa ufahamu wa matatizo kuelekea kwa ufahamu wa suluhisho. Kutumia mda kwa tatizo ni makosa. Kutumia mda na mawazo yako kwa suluhisho juu ya tatizo ni Ukweli. Hali hizi mbili za akili ziko kinyume na zenyewe: moja ni ya kuvunja ahadi na ingine ni ya kudumisha ahadi. Ushindi umeahidiwa nikiinuka juu, nikiweka mawazo yangu {na hisia} kwenye suluhisho, nikikataa kuzama kwenye undani wa tatizo.

Kati ya majasusi wale kumi na wawili waliotumwa kupiga ripoti juu ya nchi ya ahadi, wawili pekee ndio waliokuwa na malengo ya suluhisho na wakaleta ripoti nzuri. Majasusi hao wengine walikuwa na malengo ya tatizo kufikia pointi ya kukata tamaa.

Kama Churchill alitangaza, “Hofu ni jibu, ujasiri ni uamuzi.” “Bwana alihimiza wanafunzi wake wawe wenye hekima kama nyoka, ikimaanisha, msikubali kamwe imani ya Uhai na hisia katika mwili kunyamazisha kinyume chake, sayansi ya uwepo.” { Sayansi na afya, toleo la kwanza, ukurasa 250}

Kumi ya wale majasusi kumi na wawili “ waliweka kwenye kimya sayansi ya uwepo,” na kupata matokeo yaliyokuwa hatari. Hofu huweka kimya sauti ya malaika ambayo hushika kifunguo kwa suluhisho la kila shida inayoweza kufikiriwa na mwanadamu.

“ Tuliona majitu…..na tulijiona kama nzige, na ndivyo tulikuwa machoni mwao.” {Kitabu cha nambari 13:33} Hivyo, kama vile majasusi waliweka macho yao kwa ushuhuda wa hisia zao tano, kukata tamaa kwao kuliongezeka: hawakujiona tu kama wadudu wanaoweza kuangamizwa, lakini walifikiria maadui wao walitazama Israeli kama mawindo rahisi.

Mfano sawa wa matumizi mabaya ya mawazo inaonekana katika kizuka cha maangamizi cha mwisho cha Yohana, mahali akili za kimwili imeongeza kuonekana kwa nyoka ya mwanzo kuwa joka la unene mkuu.

Kama vile usemi;

“ Wawili waliangalia kupitia vizuizi vya gereza: mmoja akaona matope, na mwingine akaona Nyota.”

Majasusi wawili wa Israeli waliona “Nyota” – kwa majina Nguvu zote, Uwepo wote, Mwenye kujua yote na Mwenye Kutenda yote – na tatizo la “majitu” likatoweka: kwa kutokuweko kwake.